Kutimia au Kubatilika kwa Unabii;
JE, UNABII UNAWEZA KUBATILIKA? (JE BIBLIA INATUAMBIA NINI JUU YA KUBATILIKA AU KITIMIA KWA UNABII?) Bwana Yesu asifiwe sana mtu wa Mungu! Nashukuru sana Mungu kwa kunipa kibali siku ya leo kukutana nawe tena katika makala hii kwa nia ya kujifunza zaidi juu ya mambo yahusuyo "Unabii." Najua unaweza ukajiuliza, kwa nini tujifunze mambo kadhaa kuhusu unabii? Lakini inawezekana huamini katika unabii, na hivyo si jambo muhimu wewe kujua kuhusu mada hii. Au pia, kwa imani yako unaamini nyakati hizi hakuna manabii. Jambo moja ninalotaka kukuambia ni kwamba, naelewa na ninaheshimu mtazamo wako na mawazo yako juu ya hicho unachokiamini. Lakini ningependa ufahamu kwamba kuna ukweli ambao huujui kuhusiana na mada hii, ukweli ambao ukiufahamu utaondokana kabisa na mtazamo ulio nao. Bwana Yesu asifiwe sana! Sasa ili unielewe vizuri, natamani tukae chini kama watu wanaojifunza Neno la Mungu, tufungue akili zetu, na tujadili kwa pamoja huku tukiangalia Maandiko Matakatifu ...